Header Ads

EWE MWANAUME USIFANYE HAYA KWA MKEO.

Mtendee makosa yote Mwanamke ila usijaribu kuonyesha kwamba YEYE SI LOLOTE KWAKO! Kila Bin adam anapenda KUHESHIMIWA NA KUTHAMINIWA ili aweze kuujuwa UTU wake, Unapo mnyanyasa Mwanamke huku ukijinadi mbele ya jamii na ndugu kwamba ni MKEO WA NDOA ni sawa na kumvisha mbuzi kengele๐Ÿ•ญ
Hakuna Mwanamke atakupenda na kukuheshimu ikiwa wewe mwenyewe huijui nafasi yako kwake... Mwanamke anapenda zaidi kuwa SALAMA kuliko hata kupendwa, Maana kumtamkia NAKUPENDA wakati muda wote unaishi nae kama KIJAKAZI CHAKO wallah usije shangaa ukapewa heshima ya MUME wa cheti na Mume wa watoto, Halafu huko nje akapatikana MUME/KIONGOZI wa Furaha na Amani ya Mkeo! Sasa usijifanye kidume kwa karatasi ama hizo mbegu uliweka akapatikana mtoto eti ndo U-RELAX kama vile beberu๐Ÿ au kuku๐Ÿฆƒ wa kizungu huwiki wala hudonoi upo upooo tuuuu๐Ÿ˜‰
Ukitaka heshima ya MUME simamia nafasi yako kama Mume, Lakini ukijipa hakika ya hilo karatasi lako nenda SECRETARIAL piga lamination halafu nunua na flame ya A4 bandika sebuleni kabisaaa๐Ÿค“ ili ujifariji huku wajuao kumpa FURAHA NA AMANI MKEO wakiendelea kufaidi Mema ya MWILI.
#MAKTABATZ_kasema_ila_sio_sheria.

No comments:

Powered by Blogger.