Header Ads

Kuliko Kumkosa Shilole Kwenye Maisha Yangu ni Bora Nife- Uchebe

MCHUMBA wa staa wa mduara Bongo, Zuwema Mohamed ‘Shilole’, Uchebe Ashiraf amefunguka kuwa kuliko kumkosa Shilole kwenye maisha yake ni bora asiwepo duniani kabisa.

Akipiga mastori na MAKTABATZ, Uchebe alisema kuwa, pamoja na kwamba amegundua Shilole alirudisha mapenzi na bwana’ke wa zamani, Nuh Mziwanda lakini hayuko tayari kumuacha.

“Ninajua amenikosea sana, lakini siko radhi kumuacha, ninampenda mno na niko radhi kupoteza maisha yangu kwa ajili yake au niuze chochote nilichonacho ili tu nimridhishe atakavyo,” alisema Uchebe.

No comments:

Powered by Blogger.